CHUCHU AFUNGUKA KUHUSU WEUPE WA MPENZI WAKE RAY,KUMBE NAYE…

Chuchu Hans ameongelea weupe wa Ray
nakusema sasa amependeza kutokana na
maisha yake kubadilika kwani zamani kwake
maisha yalikuwa magumu na muda mwingi
alikuwa akitembea kwa miguu na kuhangaika
kutoka kimaisha ndiyo maana alikuwa
anaonekana vile.
“Unajua mimi huwa sipendi sana watu
wanapozungumzia suala hilo ila kwa kuwa
sisi ni watu maarufu inafika mahali unaamua
kupotezea tu, unajua watu wanashindwa
kuelewa kuwa maisha yamebadilika na saizi
sanaa ina lipa ndiyo maana Ray Kigosi
amebadilika na kutakata, unajua zamani
maisha hakuwa na uwezo sana na alikuwa
anahangaika na kutoka na muda mwingi
alikuwa akitembea kwa miguu ndio maana
alikuwa akionekana vile” Alisema Chuchu
Hans
Kwa upande wake Ray Kigosi alikiri kuwa
sasa amebadilika na kuwa mweupe na
kusema siri kubwa ni yeye kunywa maji
sana, kufanya scrub ndiyo maana amekuwa
hivyo ila hajichubui kama ambavyo watu
wanasema.

Previous
Next Post »

Ads Inside Post