Ushahuri Bora kuhusu Mambo ya Kufanya juu ya Simu yako ya zamani

Baki Nayo: Usiiuze
Kwa haraka haraka uwezi kuona kama kuna sababu ya kutoiuza – ukijiuliza ‘Utaifanyia nini sisi?’. Simu yako ya zamani unaweza ipa kazi mpya;
Kama hakuna simu ya nyumbani inayoweza tumiwa na mtu yeyote kwa ajili ya kupiga simu nyumbani basi igeuze simu hiyo kuwa ya matumizi ya nyumbani.
Simu ya dharula – igeuze kuwa simu dharula, kwa ajili ya kukusaidia pale simu yako kuu ikiharibika, kupotea n.k.
Igeuze MP3 Player , itumie kwa ajili ya kuweka na kucheza mziki kwenye gari au kwa kuunganisha na spika yako nyumbani.
Igeuze Wireless (WiFi) Router – simu janja nyingi za kisasa zinauwezo wa kurusha intaneti (tethering), basi unaweza weka laini spesheli kwa ajili ya matumizi ya intaneti na hivyo kutumia simu hiyo kama modem au WiFi router nyumbani kwako.
Mpe mtu mwingine wa karibu.
Ndio, angalia katika watu wako wa karibu kama kuna ayaeitaji simu. Unaweza mpa kama zawadi, ata kama imechakaa utashangaa mtu anayeitaji atakavyoifurahia.
au Umeamua Kuiuza…
Inawezekana ni simu ya gharama sana na ungependa kurudisha pesa uliyotumia katika ununuzi na utunzaji wa simu hiyo. Na kizuri kama ufahamu ni kwamba ata kama simu ni mbovu kuna unaoweza wauzia.
Kwenye Facebook Groups – Deals in Dar n.k, unaweza ukapost picha ya simu yako na bei kwenye makundi ya Facebook yanayounganisha watu wanaouza na wanaofuatilia vitu vinavyouzwa.
Mitandao kama ZoomTanzania , Kupatana n.k – Pia unaweza tangaza kwa urahisi kupitia mitandao kama Zoom Tanzania
Fika kwenye duka la wauza simu zilizotumika karibu yako. Hii ni njia nyingine rahisi ya kuuza simu yako, unaweza fika katika duka la wauza simu za used na ukaongea nao kuona kama wanaweza kununua simu yako
Pia unaweza ata waambia marafiki wa karibu ya kwamba unauza simu yako, unaweza kuta kuna mtu ambaye anaweza akawa tayari kuinunua.

Previous
Next Post »

Ads Inside Post